Posts

Showing posts from April, 2021

KUJUA SIYO KUTENDA, TUJITATHIMINI

Na; Mashaka J. Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Ukienda kanisa lolote lile lazima utakutana na watu wa aina tatu. Wale walio moto kwenye masuala ya kikanisa, wale ambao ni vuguvugu na wale ambao ni baridi kabisa.  Watu ambao wako moto kwenye masuala ya kikanisa, wao hushiriki katika kila shughuli ya pamoja, huweza kuhamasisha na kuwatia moyo wengine ili waweze kushiriki pia, hawa hawakati tamaa na ni waaminifu sana kwenye masuala ya kiimani japokuwa kuna changamoto za kiubinadamu pia. Mara nyingi hawa huwa ni viongozi. Watu ambao ni vuguvugu, wao husubiria hamasa kwenye kila jambo ili waweze kushiriki katika shughuli fulani. Wao husubiri watengenezewe mazingira ya urahisi au ugumu wa jambo fulani ndipo waamue kama waliunge mkono au walipige kipepsi. Hawa watu mara nyingi wanahoji sana. Kwa mfano, kiongozi yeyote yule wa kanisa anapotangaza maombi ya mfungo wa wiki m...

MIMEA HUHITAJI MIZIZI ILI KUKUA; BINADAMU TUNAHITAJI WATU ILI KUFANIKIWA

Na; Mashaka J. Siwingwa     +255764987588 ___________________________________________________________________________________ Ili mimea iweze kuota, kukua na kustawi vizuri inahitaji mizizi imara na yenye uwezo wa kustahimili ukame wakati wa dhiki. Mizizi huisaidia mimea kuweza kufyonza maji katika umbali mrefu hatimaye kuusaidia mmea kuendelea kuishi. Kustawi kwa majani na matawi ya miti ni matokeo ya kazi ngumu inayofanywa na mizizi ambayo hata hivyo siyo rahisi kuiona, kwa sababu hupatikana ardhini. Mizizi haihitaji kujionesha ili kufanya kazi ya kufyonza maji na kuyasaidia majani kustawi. Wakati mwingine ni kwamba, mizizi inapata shida sana kutafuta maji katika umbali mrefu hasa wakati wa ukame. Naam... mizizi hustahimili dhiki zote hizo. Binadamu na wanyama wengine wapitapo kando ya mimea hiyo hufurahia kuiona ikiwa imestawi vizuri bila kujua kama kuna kitu kinaitwa mizizi kinafanya kazi chini kwa chini. Mizizi haihitaji shukrani ya binadamu wanaopata kivuli ili kuendelea...

KAULI YA "LETA KAMA TULIVYO" INAVYOLIGHARIMU TAIFA LETU

Na; Mashaka J. Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Ninajua unaweza kucheka baada ya kusoma kichwa cha andiko hili. Ni kweli, kinaweza kuwa kinachekesha lakini hebu kunywa maji kidogo halafu tuendelee. "Lete kama Tulivyo" ni kauli ambayo imezoeleka na kuwa ya kawaida sana kwenye taifa letu. Sijajua kama na mataifa mengine yanaathiriwa na vitu vya ajabu namna hii lakini ngoja tujielimishe sisi wenyewe kwanza. Kauli hii imekuwa ikitumiwa sana na watu wa rika moja, wenye mambo yanayoendana, wenye elimu zinazoendana tena ambao kwa namna moja ama nyingine wanakuwa ni marafiki wa karibu sana. Tatizo si wao kuwa na umri sawa, kuwa na kiwango sawa cha elimu wala kuwa marafiki wa karibu sana. Shida ni muktadha ambao kauli hii imekuwa ikitumika. Kuna rafiki yangu mmoja nilisoma naye shule moja. Siku moja akawa ananisimulia kuhusu mzazi wake. Kwamba mzazi wake alikuwa anasumb...

KAMA HUJAFANYA KITU HUWEZI KUWA NA CHA KUPOTEZA

Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Ninajua watu wengi huwa tunaumia sana tunapopoteza vitu vyetu vya thamani. Wakati mwingine tunapoteza vitu ambavyo huwa tunaamini pengine bila vitu hivyo hatuwezi kufika popote. Vitu hivyo vyaweza kuwa ni kama vile wapenzi, mali, mitaji, jamaa zetu wa karibu, na kadhalika. Mara nyingi tunapopoteza vitu hivi huwa tunaamua kukata tamaa na kuamini kwamba kamwe havitatokea tena vitu kama hivyo kwenye maisha yetu.  Ni kweli kabisa, uthamani wa vitu hivi huwa unatufanya tuamini kwamba hatutapata vitu vingine mbadala wa vitu hivyo. Hii ni kutokana na ukweli kwamba uthamani wa vitu hivi haumithilishwi na kitu kingine chochote kile. Ni vitu maalumu na vya kipekee sana kwenye maisha yetu. Lakini, kumbuka kuvunjika kwa mpini si mwisho wa kilimo. Mpini unaweza ukavunjika na bado ukaendelea kupalilia kwa kung'olea nyasi kwenye shamba la...

MIPANGO NI MATANGO; UKIILAZA ITAOZA

 Habari yako mpenzi mfuatiliaji wa makala kutoka katika blogu hii. Napenda nikukaribishe tena kusoma makala hii ya leo. Makala ya leo ni fupi sana lakini iliyobeba ujumbe. Naam, pengine umewahi kuweka mipango yako ambayo umeona ni vema kama ukiitimiza ndani ya muda fulani. Labda ni ndani ya mwezi, miezi kadhaa, mwaka au baada ya miaka kadhaa. Napenda kukuthibitishia tu kwamba muda unakwenda na wala haurudi. Siku nazo zinazidi kusonga mbele kiasi kwamba usipokuwa makini utajikuta umefika mwisho wa malengo yako na hujafanya chochote. Ninakushauri tu upange malengo ya muda mfupi kabla ya kufikia malengo ya muda mrefu. Unaweza kuanza kwanza kupanga malengo yako kwa siku, mwezi na hata mwaka. Njia hii itakusaidia kurahisisha mipango yako ili usije kufikia siku ya mwisho hujafanya chochote. Lazima uwe na mbinu mbadala za kufikia malengo yako. Ahsante sana. Imeandikwa na; Mashaka J. Siwingwa.

YAFAHAMU MAMBO YASIYODHIHIRISHA UZALENDO

Na; Mashaka J. Siwingwa. Askofu Sylvester Gamanywa ni mchungaji na Askofu mkuu  wa kanisa la Wapo Mission International nchini Tanzania. Askofu Sylvester Gamanywa, pia, ni mwandishi wa vitabu. Moja ya vitabu vyake maarufu ni hiki cha "Uzalendo na Falsafa ya Mamlaka."  Kwa mujibu wa Askofu Sylvester Gamanywa, kitabu chake kimegawanyika katika sura kuu sita. ambapo; -Sura ya kwanza inahusu "Uzalendo kwa nchi kwa mujibu wa Biblia" (uk. 2). -Sura ya pili inahusu "Mafanikio ya Serikali ya Tanzania awamu ya tano" (uk. 23), -Sura ya tatu inahusu "Mfumo wa Demokrasia ya Tanzania" (uk.106), -Sura ya nne inahusu  "Historia na Chimbuko la Mamlaka" (uk.144), -Sura ya tano inahusu "Itifaki ya Mamlaka na Mifumo Yake" (uk. 172), na, -Sura ya sita inahusu "Chimbuko la Uasi na Mifumo Yake" (uk.218). Katika sura ya kwanza ya kitabu chake ambayo inaanza ukurasa wa pili, na ule ukurasa wa tatu ndipo mwandishi anapoorodhesha mambo kadhaa...

JIANDAE KUKABILIANA NA HII CHANGAMOTO POPOTE PALE.

 Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Mafanikio yanasogeza karibu maadui, jiandae kukabiliana nao!  Daima watu hutumia watu kuwainua watu, lakini pia watu hao hao hutumia watu kuwashusha watu...Kuwa makini, usiwaamini 100%. Kama ilivyo kawaida kwa binadamu yeyote yule akifanikiwa, marafiki huwa ni wengi sana. Wengine hudiriki hata kujigamba huko kwamba bila wao pengine usingelifika hapo ulipo. Mafanikio husogeza karibu maadui, jiandae kukabiliana nao. Muda mwingine watu wengi watakuja kutaka msaada kutoka  kwako hata wale ambao unaamini kwamba wao ndiyo wanaotakiwa kukusaidia wewe, lengo lao kubwa ni kutaka kukujaribu tu. Mafanikio husogeza karibu maadui, jiandae kukabiliana nao. Ninakumbuka bwana Justin Lupa, mmiliki wa kampuni ya kijasiriamali ya 'Canaan Trading Group Company' iliyopo Mbeya-Tanzania, wakati anaanza kuzalisha bidhaa zake za kijasir...