Posts

JE, UNACHANGAMOTO YA RATIBA ZAKO? (USIPITE BILA KUSOMA HII)

Ukipanga kukutana na mtu muda fulani, muda huo ukifika na haujakutana naye, baadaye ukimtafuta utamsikia akisema "muda umebana ndugu" au "ratiba ngumu sana aisee!" Ratiba zetu zinabana sana... Hii ni kweli kabisa. Pengine hali kama hii huwa inakupata hata wewe! Unajiona kabisa kwamba hauna muda wa kufanya jambo fulani, lakini ukiangalia kwa makini hata huo muda ulionao sasa hivi hakuna kitu cha maana unachokifanya.   Hebu fikiria, leo unaamka saa kumi na mbili kamili asubuhi halafu kesho unaamka saa mbili kamili asubuhi, kesho kutwa unaamka saa moja na nusu kisha mtondo unaamka saa kumi na moja kamili asubuhi.  Yaani ratiba zako zinakuwa shaghala baghala! Mbaya zaidi ni kwamba siku ambayo unaamka saa mbili kamili asubuhi unakuta ndiyo siku ambayo una shughuli nyingi za kufanya kuliko siku unayoamka saa kumi na moja kamili alfajiri. Tafakari tatizo liko wapi?  Ratiba zetu wengi zimekuwa na mkanganyiko sana hasa pale tunaposhindwa kugundua vipaumbele vyetu kwenye rati...

MATATIZO YA UBUNIFU, KUKOSA MIKAKATI NA UVIVU WA KUFIKIRI MATOKEO MAKUBWA VINAVYOTUTAFUNA

Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Sina shaka na uwezo binafsi wa kufikiri kwako na nina imani kabisa wewe ni mtu ambaye umejaaliwa uwezo mwema kabisa wa kufikiri.  Pamoja na kwamba una uwezo mzuri wa kufikiri, unaweza kukuta mambo yako hayaendi kwa sababu ya kitu kimoja tu ambacho mpaka leo bado hukielewi! Wakati mwingine unaweza kukuta ni kweli kabisa unajitahidi kujituma, mathalani unapambana sana kuongeza kipato chako kwa kufanya biashara yako, kulima kadri uwezavyo, kuzamiria baharini kwa bidii lakini cha ajabu kila unapolima matokeo ni yaleyale, kila unapofanya biashara matokeo ni yaleyale, kila unapovua matokeo ni yaleyale.  Najua inaumiza sana kwa mtu yeyote yule kufanya biashara ambayo faida yake haionekani ama ni kiduchu hasa pale anapokuwa anajitahidi kufanya jambo hilo kwa bidii akitegemea kupata zaidi lakini mwisho wa siku anaishia kuvuna k...

AHADI KUMI ZITAKAZO KUFANYA UFIKIE NDOTO ZAKO MWAKA 2021( TOLEO LA PILI)

Mashaka J. Siwingwa       (Mzumbe University)           +255774987588 _______________________________________ Kwanza kabisa tumshukuru mwenyezi Mungu atupaye uzima na afya kwa kutuvusha salama kutoka mwaka 2020 na kutuleta katika mwaka wa mipango mingi wa 2021. Inawezekana mwaka 2020 haukuwa wa furaha kwako, haukuwa wa mafanikio kwako, mambo mengi uliyopanga hayakufanikiwa. Naomba tunapokwenda kuuanza mwaka mpya ukajiwekee ahadi zifuatazo wewe mwenyewe bila kusukumwa na mtu. Ahadi hizi zitakusaidia kukupa nguvu, kukutia moyo pamoja na kukutoa hofu kwa mipango ambayo umekwisha kujipangia au unataka kujipangia.  Ni matumaini yangu, ahadi hizi zitafanyika msaada kwako na kuwa mwanga wa matumaini na mafanikio kwako:- 1. Jiahidi wewe mwenyewe kuwa imara kiasi kwamba hakuna kitu kinachoweza kuutikisa ufahamu wako. Katika maisha kuna changamoto nyingi sana ambazo zinasimama kama vikwazo katika mafanikio yako. Kuna magonjwa, mikosi, kudharauliwa pamo...

UNAVYOPISHANA NA FURSA KWA KUOGOPA MASOMO FULANI

Ninajua unajua ila unajifanya hujui... Sitaki kukufanya ujue ila kukusaidia unavyoweza kujua! Kwenye kila kitu anachokisomea mtu, kina fursa zake bila kujali ni za kuajiriwa ama hata kujiajiri. Watu wengi sana katika jamii zetu wamekuwa wakijidharau kwa kuona kwamba kitu wanachokisomea ni dhaifu na kuona kwamba wapo katika giza nene la kutokutambua kama kitu hicho kinaweza kuwatoa kimaisha au la! Hii no kutokana na sababu kadhaa ambazo ni sambamba na; kutopenda kitu unachokisomea kutokana na sababu za wewe kusoma kozi hiyo ambazo aidha ni ufaulu wako ulikushinikiza kuisoma ama ni kulingana na hali ya maisha ya nyumbani kwenu. Sikiliza nikwambie, hakuna ujinga mtupu. Kila kwenye ujinga kuna fundisho hapo! Mbona hujiulizi kuhusu akina Masud Kipanya wanaoishi kwa kuchora vibonzo tu na maisha yao yanasonga mbele? Wanakula na kusomesha watoto shule nzuri tu? Sema tu ni vile  wewe ni mzembe wa kufikiri... Katika ulimwengu huu wa leo, zipo taaluma ambazo kwakweli wanajiona ni watu dhaifu ...

HAUHITAJI ELIMU KUBWA SANA ILI KUFANYA MAGEUZI KWENYE MAISHA YAKO.

________________________________________ Ni ukweli usiopingika kwamba elimu ni muhimu; tena sana hasa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia. Elimu ndiyo inayokusaidia kutengeneza mifumo ya kujiongezea kipato hasa kwa kutumia maendeleo ya sayansi na teknolojia. Kupitia elimu uliyonayo, unaweza kutumia mitandao ya kijamii kutangaza biashara yako, kutoa mafunzo yako kwa watu na kuwashirikisha wengine fursa ya kimaisha uliyoweza kuichungulia. Elimu yangu ndiye kiungo mkubwa na aliyebeba dhamana ya mafanikio yako. Zaidi ya elimu, uelewa na ufahamu wako. Sambamba na hayo yote, ni dhahiri kwamba wakati mwingine mafanikio hayahitaji elimu kubwa sana kama wengi wanavyodhani, japokuwa kuna njia mbalimbali za kusaka mafanikio; elimu kubwa ikiwemo. Hatuwezi kuubeza mchango wa elimu katika mchakato mzima wa kusaka tonge. Naam, unaweza kujipima mwenyewe kama elimu uliyonayo kwa wakati huu inaweza kukusaidia kuingiza mkono kinywani, la sivyo endelea kupambana! Elimu ifanyike kuwa mkombozi wa ...

ONA UNAVYOPISHANA NA FURSA KWA KUOGOPA!

"Ni vile tu wewe siyo mbunifu!"   Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Ninajua unajua ila unajifanya hujui... Sitaki kukufanya ujue ila kukusaidia unavyoweza kujua!  Imekuwa ni kawaida kwa ndugu, jamaa au marafiki zetu kudharau au kuboza taaluma fulani. Mathalani hata wewe pia umewahi kufikiri juu ya suala la kuibeza taaluma fulani au kuwabeza watu fulani. Hakuna ujinga mtupu na kwenye kila kitu anachokisomea mtu, kina fursa zake bila kujali ni za kuajiriwa ama hata kujiajiri. Watu wengi sana katika jamii zetu wamekuwa wakijidharau kwa kuona kwamba kitu wanachokisomea ni dhaifu na kuona kwamba wapo katika giza nene la kutokutambua kama kitu hicho kinaweza kuwatoa kimaisha au la! Sikiliza nikwambie, hakuna ujinga mtupu. Kila kwenye ujinga kuna fundisho hapo! Mbona hujiulizi kuhusu akina Masud Kipanya wanaoishi kwa kuchora vibonzo tu na maisha yao yanasong...

NI MUHIMU SANA KUSHUKURU KWA NAMNA ULIVYO

...wakati tunafurahi upande wa kusi, waliopo kasi wanalia...! Naam imekuwa desturi kabisa kwa watu kufurahia maisha kwa 'kula bata' pale tunapokuwa na afya bora. Mara nyingi tumekuwa tukiwaarika marafiki zetu kuhudhuria 'Night Clubs' na kufurahi pamoja nao. Wakati mwingine tumewagharamia wapenzi wetu kwa kuwanunulia zawadi kabambe na zenye gharama fikirishi!  Sijasema ni jambo baya la hasha! Bali ni desturi tu ambazo kama binadamu tumejijengea. Siku moja nilifanikiwa kununua gazeti moja na kupitia-pitia habari kedekede zilizokuwa zimeandikwa gazetini humo huku zikihaririwa na wataalamu nguli! Nilivyoufikia ukurasa wa sita wa gazeti hilo nikakutana na kichwa cha habari  kikubwa kimeandikwa, "MREMBO ateseka miaka 5 kitandani, achungulia kaburi." Kichwa cha habari hiki kilishadidiwa kwa maandishi meusi tii tena hata picha ya msichana mmoja iliyokuwa imeambatanishwa na ujumbe huu, hata hivyo nilishindwa kung'amua vizuri muonekano wake kutokana na picha yake ku...