Posts

Showing posts from December, 2020

KILA MTU NI GENIUS; JE, WEWE NI GENIUS WA KITU GANI?

"Everyone is a genius but if you judge a fish by it's ability to climb a tree, it will live its whole life believing that it is stupid". Hii ilikuwa ni kauli ya Albert Einstein akiwa na maana ya kwamba; " Kila mtu ni genius, lakini kama ukimhukumu samaki kwa kushindwa kupanda juu ya mti basi ataishi maisha yake yote akiamini kwamba hana akili". Mungu alipokuleta duniani, alihakikisha kwamba ameweza kuweka uwezo wa pekee sana ambao mara tu utakapougundua na kuanza kuufanyia kazi utakuletea matokeo makubwa sana. Watu wengi wanazaliwa na hadi wanaondoka duniani hawajajua uwezo wao huu wa kipekee uliojificha ndani yao na matokeo yake wanaishia kuwa watu wa kawaida sana. Ndiyo maana unawakuta watu wengi wanakata tamaa wakifeli masomo na mitihani mbalimbali. Mathalani hata jamii umekuwa ikiwazomea kwa kushindwa katika mitihani hiyo! Mbona hujiulizi kwanini watu wengi waliofanikiwa hawakuwa na uwezo mkubwa darasani? Moja ya hatari kubwa sana ya kutojua uwezo wako ni ku...

USIOGOPE, WEWE SI WA KWANZA KUWEKEWA VIKWAZO.

Tangu mnamo mwaka 1917 nchi ya Marekani imekuwa ikiliwekea vikwazo kadhaa vya kiuchumi taifa dogo la Cuba. Baadhi ya mikataba mbalimbali ilisainiwa ili kumuondoa Cuba kwenye ramani ya ushindani kiuchumi lakini mpaka leo bado anadunda tu! Kwa uchache tu, mikataba hiyo ni kama vile:  -Trading with the Enemy Act of 1917. -The Foreign Assistance Act of 1961. -The Cuban Assets Control Regulations of 1963. - The Torricelli Act of 1992. -The Helms-Burton Act of 1996 - The Trade Sanction Reform and Export Enhancement Act of 2000. - The U.S Commission for Assistance to a Free Cuba of 2004 and 2006. Naomba kunukuu kidogo hapa; " According to the U.S government... The embargo on Cuba is the most comprehensive set of American sanctions ever imposed upo  a country. (The Economic War Against Cuba_ A Historical and Legal Perspective on the U.S Blockade ,2013). Hapo juu ni baadhi tu ya mikataba iliyosainiwa ili kumuwekea vikwazo Cuba lakini mpaka leo bado anatikisa tu mtaani. Historia inaonye...

KUELEKEA 2021, JIWEKEE AHADI JUU YA HAYA MAMBO KUMI

Natambua kwamba tupo mwishoni mwa mwaka 2020 na tunakwenda kuupokea mwaka 2021 hivi punde. Inawezekana mwaka 2020 haukuwa wa furaha kwako, haukuwa wa mafanikio kwako, mambo mengi uliyopanga hayakufanikiwa. Naomba tunapokwenda kuingia mwaka mpya ukajiwekee ahadi  zifuatazo wewe mwenyewe bila kusukumwa na mtu. Ni matumaini yangu, ahadi hizi zitafanyika msaada kwako: 1. Jiahidi wewe mwenyewe kuwa imara kiasi kwamba hakuna kitu kinachoweza kuutikisa ufahamu wako. 2. Jiahidi wewe mwenyewe kuwa mtu mwenye afya, amani, mafanikio na furaha kwa mtu yeyote utakayekutana naye maishani mwako. 3. Jiahidi wewe mwenyewe kuwafanya marafiki zako kwamba kuna kitu wanacho katika fahamu zao, hawako watupu. 4. Jiahidi wewe mwenyewe kufanya yaliyobora, kwa kufiri kwa namna iliyobora na kwa manufaa bora. 5. Jiahidi wewe mwenyewe kujifunza kupitia mafanikio ya wengine huku ukiamini kwamba na wewe upo njiani kufanikiwa. 6. Jiahidi kusahau makosa ya zamani huku ukitarajia kupata mafanikio makubwa sana mbele...

TUNAKWAMA WAPI?

Image
Mada ya Promotion of Life Skills hufundishwa tangu kidato cha kwanza katika somo la Uraia (Civics). Ni moja ya mada tamu sana na zinazogusa moja kwa moja maisha yetu ya kawaida. Mada hii inapofundishwa ina vipengele mbalimbali. Moja ya vipengele hivyo ni kile kinachosema, Steps of Problem Solving (Hatua za kutatua matatizo). Hapa utakuta wanakwambia hatua namba moja ni Identification of a problem (Utambuzi wa tatizo). Yaani kabla hujaanza kupambana na changamoto hiyo anza kwanza kwa kuitambua changamoto hiyo. Halafu mada hii inajirudia tena kidato cha tatu ikiwa na jina lile lile, vipengele vile vile, lakini visiki vya mpingo mimi na wewe bado tunakwama; aaah tunakwama wapi? Mwimbaji wa nyimbo za injili Martha Baraka mnamo tarehe 24 mwezi wa nane mwaka 2018  aliimba kibao chake kinachoitwa "Nini chanzo?" Katika kibao hiki amewagusa watu kadhaa katika historia ya imani ya kikristo, moja ya watu hao ni akina Anania na Safira ambao hadithi yao inapatikana katika kitabu cha Maten...

MATATIZO NI KAMA SAA YA MSHALE

Image
Imekuwa ni desturi sasa watu kununua saa za mkononi kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya kuangalia muda. Wakati mwingine watu hawa wananunua saa za bei ghari ili kuzionesha kwa watu (show off). Waathirika wakubwa wa tatizo hili ni sisi vijana. Ndiyo! Hata mimi ninapenda show off! Siku hizi si ajabu kumkuta kijana wa kipato cha kawaida kabisa akijipinda na kununua saa ya shilingi za kitanzania elfu hamsini! Unafikiri lengo lake ni kuangalia muda? Je, sisi tunaonunua saa za shilingi elfu moja na miatano hatuwezi kuangalia muda?  Tuweke hayo kando! Nakumbuka kipindi nikiwa mtoto mdogo wa darasa la tatu, niliwahi kununuliwa saa ya shilingi za kitanzania elfu moja na miatano na baba yangu. Nilifurahi mno! Nilivyofika darasa la tano nikawa na uwezo wa kununua saa yenye thamani ya shilingi za kitanzania elfu tatu. Hii nayo ilikuwa ni ya kuhesabu kama stop watch! Baadaye nikaona mwenyewe sasa nimekua mtu mzima, sistahili kumiliki saa ya namna hiyo. Hapo ndipo nilipoamua kununua saa ya mshal...