Posts

Showing posts from June, 2021

UKITAKA WATU WAKUHESHIMU FANYA HIVI

Kila mtu anastahili kupewa heshima na kuthaminiwa. Hii ni kutokana na ukweli kwamba heshima na thamani ni kitu ambacho kila mtu anastahili. Haijalishi elimu zetu, tamaduni zetu, makabila yetu, dini zetu wala maeneo tunayotokea. Kutokuheshimiana ni moja ya kitu ambacho kimekuwa kikisababisha migogoro kwa watu mbalimbali. Mtu mmoja anaposhindwa kumheshimu mwenzake hupelekea migogoro na hata kuvunja ukaribu wao. Marafiki wawili wanaposhindwa kuheshimiana huwa hawana haja tena ya kuona kama urafiki wao una manufaa yoyote yale bali huamua kuvunja urafiki wao. Wapenzi wengi pia wanaposhindwa kuheshimiana hupelekea mogogoro kwenye mapenzi yao na hata kuvunja mahusiano. Mathalani, wanandoa wanaposhindwa kuheshimiana na kuthaminiana hupelekea  migogoro ndani ya nyumba na hatimaye kuamua kuvunja mahusiano au ndoa yao. Kwa kawaida, suala la kutoheshimiana ni suala la mtu mmoja mmoja kwani ni matokeo ya ubinafsi baina yetu. Kwa mujibu wa Dkt. Issaya Lupogo & Aziza Lupogo (2019) katika kita...

SAA ZA KIBONGO DHIDI YA SAA ZA KIZUNGU: WABONGO TUNAZINGUA SANA

Na: Mashaka Siwingwa __________________________________________ "Do you love life? Then do not squander time; for it is the stuff that life is made of." Ilikuwa ni kauli ya Benjamin Franklin kama alivyonukuliwa na Brian Tracy katika kitabu chake cha Time Power. Siku hizi wabongo tumetumbukia katika balaa; naam balaa zito kwelikweli. Balaa la kushindwa kuwa na nidhamu; nidhamu katika matumizi ya muda. Siku hizi kuna muda wa kibongo na muda wa kizungu. Mtu akikwambia tukutane saa saba kamili saa za kibongo basi ujue hiyo ni saa tisa kama siyo saa kumi na nusu. Mtu akikwambia tukutane saa nane kamili saa za kizungu basi ujue hiyo ni saa nane kamili kama ilivyotajwa. Hizi kauli za "saa za kibongo"  na "saa za kizungu"  tumezitengeneza wenyewe aidha kwa kujua au kutokujua. Tumekuwa tukiwaabudu wazungu bila kujua kwa sababu tunakubali kila kilicho cha kwao.   Saa za kibongo ni ishara ya dharau na kukosa uaminifu wakati saa za kizungu ni uaminifu na "commitm...

"MUUZA KIFO AFARIKI DUNIA"

Kaka wa mtengeneza silaha maarufu duniani, Alfred Nobel alifariki dunia na waandishi wa habari wakaibuka na kuandika, "Muuza Kifo Afariki Dunia"  Awali, waandishi wa habari waliamini kwamba aliyefariki ni Alfred Nobel ambaye alikuwa ni mtengeneza mabomu na silaha za moto kwa kutumia madini ya dainamaiti. Alfred Nobel alikuwa mtengenezaji mabomu wa dainamaiti na alifanya kazi hiyo kama sehemu yake ya kujiingizia kipato. Ulimwengu ulimchukia kwa sababu aliuza kifo na kwa bahati mbaya hakufanikiwa kung'amua kitu cha namna hii.  Alfred Nobel aliishi maisha ya furaha sana kwa kuwa na kipato kizuri kupitia kuuza silaha hizo hatari. Kwa bahati mbaya ni kwamba hakufanikiwa kujua namna ambavyo alikuwa anachukiwa na jamii yake kwa kazi hiyo haramu. Baada ya miaka kadhaa kupita, kaka yake alifariki na waandishi wa habari baada ya kupata habari hizo wakajua aliyefariki ni Alfred aliyekuwa akitegemea kazi ya kutengeneza mabomu na silaha kama sehemu yake ya kujiingizia kipato. Waandish...