Posts

Showing posts from August, 2024

Fahamu Kwa nini Unapaswa Kujenga Tabia ya Kujisomea Vitabu (Faida za Kujisomea Vitabu)

Image
(Sehemu ya Pili) Habari... Mara ya mwisho tuliangazia sehemu ya kwanza ya somo hili ambapo tuliangalia kwa utondoti sababu za kwa nini watu hawapendi/hawana utamaduni wa kujisomea vitabu. Moja ya sababu ambayo tuliangalia ni watu kutojua umuhimu wa kujisomea vitabu.   Basi leo katika sehemu hii natamani tujue faida za kusoma vitabu pengine tunaweza kuwaamsha baadhi ya wenzetu na kuwatia hamu ya kusoma. Zifuatazo ni faida za kujisomea vitabu; >> Kuongeza Maarifa: Vitabu ni chanzo kikuu cha maarifa na taarifa. Kusoma vitabu kunakuwezesha kujifunza mambo mapya na kuongeza uelewa wako wa ulimwengu. >> Kuboresha Uwezo wa Kufikiria: Kusoma vitabu kunachochea ubongo kufanya kazi, hivyo kuboresha uwezo wako wa kufikiria kwa undani, kutatua matatizo, na kufanya maamuzi bora. >> Kuboresha Lugha na Msamiati: Kusoma vitabu husaidia kuboresha uwezo wa lugha, kuongeza msamiati, na kuelewa matumizi sahihi ya maneno. >> Kuongeza Uwezo wa Kujieleza: Kusoma vitabu kunasaidia ...

KWA NINI WATU WENGI HAWANA UTAMADUNI WA KUJISOMEA VITABU?

Image
 Kwa Nini Watu Wengi Hawana Utamaduni/Hawapendi Kujisomea Vitabu?  (Sehemu ya Kwanza) Habari... Siku kadhaa zilizopita niliandika kwenye kurasa zangu za mitandao ya kijamii mara baada ya kufanya kipindi cha 'The Fix' cha redio kuhusiana na mada inayosema 'Kwa Nini Watu Wengi Hawapendi Kusoma Vitabu?' Nakumbuka baada ya chapisho lile niliahidi kukufikishia somo lote hatua kwa hatu. Sasa leo natamani somo hili liwe kama sehemu ya kwanza na mada ile ile ambapo leo tutaangalia sababu za watu wengi kutokuwa na mwamko, shauku ama utamaduni wa kujisomea vitabu. Zifuatazo ni baadhi tu ya sababu za watu wengi kutokuwa na utamaduni wa kujisomea vitabu; >> Mabadiliko ya Teknolojia (Simu na Mitandao ya Kijamii); Vifaa vya kisasa kama simu za mkononi, kompyuta, na mitandao ya kijamii vimechukua nafasi kubwa katika maisha ya watu. Watu wengi wanapendelea kutumia muda wao kwenye mitandao badala ya kusoma vitabu. >> Video na Habari za Papo kwa Papo; Watu wanaweza kupata hab...

Mbwa Bado Hajafa! (Usikubali Kukata Tamaa)

Image
Meshack Siwingwa 0764 987 588 Jamaa mmoja alikuwa akisafiri kutoka nyumbani kwake kuelekea mjini majira ya saa moja asubuhi. Baada ya mwendo wa kama saa mbili hivi alikutana na kijana mmoja akiwa amesimama barabarani akingojea kumwona mtu aendaye mjini ili aweze kumuomba 'lift.' Kijana huyu alikuwa amebeba vifaa kadhaa vinavyotumika kwa ajili ya usafi wa kuoshea magari vile ambavyo alivimudu kuvibeba. Kando ya huyu kijana alikuwa amelala mbwa aliyeonekana kuwa dhooofu bin hal kwani alikuwa akitweta kwa uchungu uliosababishwa na maumivu aliyokuwa nayo. Yule kijana alipunga mkono kwa jamaa ndipo jamaa aliposimamisha gari yake na kuamua kumsikiliza kijana. Kijana alimweleza jamaa kwamba alikuwa anaelekea mjini kumtibia mbwa wake na kwamba baadhi ya vifaa kadha alivyokuwa navyo alitegemea apate kazi za kuosha magari pindi afikapo mjini ili aweze kupata fedha za kumudu gharama za matibabu ya mbwa wake. Jamaa alishangaa sana baada ya kuona hali ya mbwa wa yule kijana na ndipo alipoam...