Posts

Showing posts from August, 2021

HIVI NDIVYO TUNAVYOWEZA KUSAPOTI WAHITIMU WAPYA KUANZISHA BIASHARA

Na:- Mashaka Siwingwa +255764987588 ____________________________________________________________________________________ Mnamo Juni 2021, niliweza kupokea kadi za aina tatu tofauti tofauti. Ninaweza kusema kwamba ulikuwa ni mwezi wa neema sana kwangu kiasi kwamba nilithaminiwa mpaka kufikia hatua ya kupewa kadi. Kadi ya kwanza ilikuwa imenakshiwa safi kabisa kwa rangi ya mzambarau. Ilikuwa ni kadi nzuri na yenye kuvuti. Ilikuwa ni kadi iliyoambatanishwa na jina langu kabisa tena kwa herufi kubwa. Baada ya kuifungua na kuisoma ilikuwa ikinitaka kuchangia harusi ya rafiki yangu ambaye alitarajia kufunga pingu za maisha Oktoba, 2021. Nilimshukuru sana Mungu kwa kitendo cha mimi kuonekana wa maana mpaka kufikia hatua ya kupewa kadi ya kuchangia harusi. Hiyo niliiweka chini. Baada ya kuiweka chini niliichukua kadi ya pili. Hii ilionekana kuwa ya hadhi ya chini kidogo na haikupambwa sana kama ile ya awali. Niliipokea kutoka kwa rafiki yangu wa karibu. Nilivyoifungua na kuisoma niligundua kwa...

TOFAUTI KUBWA ILIYOPO KATI YA UONGOZI NA CHEO

Mara nyingi watu huchanganya kati ya hizi dhana mbili. Watu wengi hudhani kwamba ziko sawa na wachache hudhani kwamba zinatofautiana. Ndiyo! Inawezekana zipo sawa au zinatofautiana kulingana na namna unavyozitafsiri dhana hizi.  Siku ya leo ninaomba niwasaidie wale wanaojua dhana hizi zinaendana 100% na hawawezi kabisa kutofautisha kati ya dhana hizi. Uongozi ni madaraka anayopewa mtu ya kusimamia au kuongoza. Au ni majukumu ambayo mtu hukabidhiwa ili ayatekeleze. Kwa upande mwingine tuna istilahi 'Cheo.' Istilahi hii ina maana nyingi kwa mujibu wa waandishi mbalimbali na kamusi mbalimbali za lugha ya kiswahili. Kwa mujibu wa kamusi moja inasema 'Cheo' ni nafasi ya hadhi ambayo mtu anapewa kazini. Lakini pia kuna maana isemayo 'Cheo' ni ubao utumikao kusukia ukili. Zaidi ni kwamba kuna tafsiri nyingi sana na nyingine ni tofauti sana na lengo letu. Sasa lengo letu ni kutofautisha dhana ya cheo kama hadhi ya heshima anayopewa mtu na uongozi kama dhamana ya majukum...