Posts

Showing posts from May, 2021

KAULI KUMI ZA HAYATI MWL. JULIUS K. NYERERE KUHUSU ELIMU NDANI NA NJE YA NCHI

Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Ni miaka mingi imepita tangu atutoke baba wa taifa Hayati, Julius Kambarage Nyerere. Ushujaa na uhodari wake katika kupambanua mambo pamoja na kueleza vitu bayana kunamfanya aendelee kuwa shujaa asiyesahaulika. Wakati wa uhai wake, baba wa taifa alisisitiza sana juu ya suala la elimu hapa nchini. Falsafa yake ya kuamini kwamba elimu ndiyo silaha pekee ya kuufikia ukombozi wa kweli hasa kifikra. Katika nyakati tofauti tofauti, katika sehemu tofauti na katika muktadha tofauti, Hayati baba wa taifa aliweza kuonesha wazi msimamo wake juu ya mfumo wetu wa elimu. Kati ya mengi aliyoyazungumza, leo nimeamua nikukusanyie kauli kumi tu alizowahi kuzitoa shujaa huyu.  Twende sawa; 1. Kauli aliyoitamka mnamo tarehe 31 Desemba, 1969 akizungumza na vyombo vya habari kuhusu malengo ya Elimu ya Watu Wazima. Alisema, "... education is som...

TABIA KUMI RAHISI SANA ZA KUFANYA ILI UANZE KUFANIKIWA

Na; Mashaka Siwingwa +255764987588 ----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------- Suala la kufanikiwa siyo tukio la sekunde moja au siku moja kama wengi wadhanivyo. Ni mchakato mrefu na wenye mfululizo wa matukio kadhaa. Hata hivyo, tulio wengi hatujui kanuni bora za kupitia ili tuweze kufanikiwa. Kwa kubeza ujumbe huu, kuna mdau anayeniona kila siku atasema mbona mimi sijafanikiwa! Shauri yako.  Ili uweze kufanikiwa unahitaji vitu kadhaa muhimu sana. Hivi vitu vitaamua hatma ya maisha yako katika nyanja mbalimbali.  Pasi na shaka, kuna mtu ataauliza kama kuna nyanja za maisha. Ndiyo, kuna nyanja mbalimbali za maisha. Kati ya hizo ni pamoja na kufanikiwa kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kadharika. Baadhi ya tabia zifuatazo zinaweza kumtengenezea mtu mazingira ya kufanikiwa moja kwa moja. Au zinaweza kuwa mwanga wa mafanikio yake. Kanuni au tabia hizo ni pamoja na; 1. Mtu anayezingatia kanu...